Ingawa imedaiwa sana kuwa Fellaini atamfuata aliekuwa Meneja wake huko Everton, David Moyes, ambae sasa yupo Manchester United, lakini uvumi huo wa Kiungo huyo kwenda Arsenal unadai kuwa Old Trafford inasita kumchukua hasa kwa sababu ya staili yake ya uchezaji iko tofauti na ile ya Klabu hiyo ingawa pia hilo hilo linaweza kusemwa kwa staili ya Arsenal.
Paris Saint-Germain baada ya kumkosa Radamel Falcao aliyekimbilia Monaco masikio na macho yao wameyaelekezea kwa Rooney pia na wako tayari kulipa kiasi cha £300k kwa wiki na tayari yupo kwenye tageti zao tangu siku nyingi imefahamika.
No comments:
Post a Comment