Tuesday 2 July 2013

HAWA NDIO WACHEZAJI WATANO WANAO WAKILISHA AFRIKA KWA KUCHEZA SOKA NA KULIPWA KIASI KIKUBWA CHA PESA


Kutoka katika orodha iliyotolea na Forbes kuonyesha wanamichezo matajiri zaidi duniani ikiwa na wanamichezo kama vile Tiger Woods kama mwanamichezo anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani - dola milioni 78.1 kwa mwaka, akifuatiwa na mcheza Tennis Roger Federer katika nafasi ya pili na Kobe Bryant katika nafasi ya tatu, Na sasa pia imefahamika ni wanasoka gani kutoka Afrika ambao wanalipwa
Hii ndiyo ile orodha iliyotolewa na Forbes hivi karibuni kuonyesha wasakata kabumbu kutoka Afrika ambao wanavuna mulla ama pesa ndefu zaidi katika kazi yao hii kutoka katika clabu mbalimbali wanazochezea.
Kwa kuanzia, katika list hii, wa kwanza kabisa ni mkali Yaya Toure, Raia wa Ivory Coast ambaye anacheza soka katika clabu ya Machester City, Kwa mwaka anaingiza Dola milioni 18.2, na mshahara wake wa wiki ni dola 320000 ambayo nnje ya bonus na allowance nyingine.




Yaya Toure
Katika nafasi ya pili yupo Samuel Eto’o kutoka Cameroon, Staa huyu anakipiga katika Clabu ya Anzhi kwa sasa, na mshahara wake kwa mwaka ni dola milioni 13.4, kwa wiki mshahara wake ni dola 300,000.



Eto'o

Wa tatu ni Didier Drogba wa Ivory Coast, kwa sasa yupo na clabu ya Galatasaray na mshahara wake kwa mwaka ni dola milioni 12.9, mpunga anaochukua kwa wiki ni dola 185,000 na pia nnje ya soka huyu ni star ambaye ana deals mbalimbali za matangazo na kampuni kama Pepsi, Nike, Samsung na Mtandao wa Orange Ufaransa.




Drogba

Mwingine ni Seydou Keita wa Mali ambaye anasakata kabumbu na clabu ya Dalian Aerbin, Mshahara wake kwa mwaka ni dola milioni 12.



Keita
Anayefuatia ni Emmanuel Adebayor kutoka Togo, Mshahara wake kwa mwaka ni dola Milioni 10, Mshahara wake kwa wiki ni dola 220,000, mbali na soka pia mchezaji huyu ana deals kadhaa za matangazo ambazo zinamuongezea mulla.


Adebayor

Tazama hichi kitu Justin Bieber alichoamua kulifanya gari lake ili tu likae 'kijanja' kama yeye alivyo vaa

Hili ndilo tukio lingine ambalo limemrudisha Mwanamuziki Justin Bieber kwenye Headlines tena, This tym round, ikiwa ni kutokana na kitendo chake cha kuamua kutoa kiasi cha paundi 125,000, ambazo ni zaidi ya shilingi 309,000,000 kwaajili ya kubadilisha rangi ya gari yake.

Bieber ameamua kuliweka gari hili rangi sawasawa na na muonekano wa 
chui, na habari za uhakika kutoka ndani ya team ya msanii huyu zinasema 
kuwa, Staa huyu aliamua kufanya  mchongo huu ili kuwezesha gari yake 
ku-match na mtoko wake wa 'kichui-chui' aliokuwa amejipanga kushine nao 
kwa siku moja.
Hivi ndio gari ya staa huyu inavyoonekana baada ya kufanyiwa mabadiliko.

RAIS WA MAREKANI BARACK OBAMA AMEREJEA MAREKANI LEO




Gari lililombeba Rais Obama likielekea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kumaliza ziara yake.



Rais Obama na mkewe michelle Obama wakipunga mikono kbla ya kuanza safari








Gari lililombeba Rais Obama likielekea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kumaliza ziara yake.

Msafala wa Rais obama ukipita maeneo ya buguruni kuelekea uwanja wa ndege