Tuesday 2 July 2013

HAWA NDIO WACHEZAJI WATANO WANAO WAKILISHA AFRIKA KWA KUCHEZA SOKA NA KULIPWA KIASI KIKUBWA CHA PESA


Kutoka katika orodha iliyotolea na Forbes kuonyesha wanamichezo matajiri zaidi duniani ikiwa na wanamichezo kama vile Tiger Woods kama mwanamichezo anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani - dola milioni 78.1 kwa mwaka, akifuatiwa na mcheza Tennis Roger Federer katika nafasi ya pili na Kobe Bryant katika nafasi ya tatu, Na sasa pia imefahamika ni wanasoka gani kutoka Afrika ambao wanalipwa
Hii ndiyo ile orodha iliyotolewa na Forbes hivi karibuni kuonyesha wasakata kabumbu kutoka Afrika ambao wanavuna mulla ama pesa ndefu zaidi katika kazi yao hii kutoka katika clabu mbalimbali wanazochezea.
Kwa kuanzia, katika list hii, wa kwanza kabisa ni mkali Yaya Toure, Raia wa Ivory Coast ambaye anacheza soka katika clabu ya Machester City, Kwa mwaka anaingiza Dola milioni 18.2, na mshahara wake wa wiki ni dola 320000 ambayo nnje ya bonus na allowance nyingine.




Yaya Toure
Katika nafasi ya pili yupo Samuel Eto’o kutoka Cameroon, Staa huyu anakipiga katika Clabu ya Anzhi kwa sasa, na mshahara wake kwa mwaka ni dola milioni 13.4, kwa wiki mshahara wake ni dola 300,000.



Eto'o

Wa tatu ni Didier Drogba wa Ivory Coast, kwa sasa yupo na clabu ya Galatasaray na mshahara wake kwa mwaka ni dola milioni 12.9, mpunga anaochukua kwa wiki ni dola 185,000 na pia nnje ya soka huyu ni star ambaye ana deals mbalimbali za matangazo na kampuni kama Pepsi, Nike, Samsung na Mtandao wa Orange Ufaransa.




Drogba

Mwingine ni Seydou Keita wa Mali ambaye anasakata kabumbu na clabu ya Dalian Aerbin, Mshahara wake kwa mwaka ni dola milioni 12.



Keita
Anayefuatia ni Emmanuel Adebayor kutoka Togo, Mshahara wake kwa mwaka ni dola Milioni 10, Mshahara wake kwa wiki ni dola 220,000, mbali na soka pia mchezaji huyu ana deals kadhaa za matangazo ambazo zinamuongezea mulla.


Adebayor

Tazama hichi kitu Justin Bieber alichoamua kulifanya gari lake ili tu likae 'kijanja' kama yeye alivyo vaa

Hili ndilo tukio lingine ambalo limemrudisha Mwanamuziki Justin Bieber kwenye Headlines tena, This tym round, ikiwa ni kutokana na kitendo chake cha kuamua kutoa kiasi cha paundi 125,000, ambazo ni zaidi ya shilingi 309,000,000 kwaajili ya kubadilisha rangi ya gari yake.

Bieber ameamua kuliweka gari hili rangi sawasawa na na muonekano wa 
chui, na habari za uhakika kutoka ndani ya team ya msanii huyu zinasema 
kuwa, Staa huyu aliamua kufanya  mchongo huu ili kuwezesha gari yake 
ku-match na mtoko wake wa 'kichui-chui' aliokuwa amejipanga kushine nao 
kwa siku moja.
Hivi ndio gari ya staa huyu inavyoonekana baada ya kufanyiwa mabadiliko.

RAIS WA MAREKANI BARACK OBAMA AMEREJEA MAREKANI LEO




Gari lililombeba Rais Obama likielekea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kumaliza ziara yake.



Rais Obama na mkewe michelle Obama wakipunga mikono kbla ya kuanza safari








Gari lililombeba Rais Obama likielekea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kumaliza ziara yake.

Msafala wa Rais obama ukipita maeneo ya buguruni kuelekea uwanja wa ndege

Sunday 23 June 2013

kocha wa arsenal ajitosa rasmi kumuwania mshambuliaji wa manchester united wayne rooney





Wayne Rooney



Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger
KLABU ya Arsenal baada ya kumalizana kwa dau la Pauni Milioni 22 na Gonzalo Higuain kutoka Real Madrid, sasa inahamishia nguvu zake kwa mshambuliaji wa Manchester United, anayeuzwa Pauni Milioni 20, Wayne Rooney - huku kocha Arsene Wenger akiwa amedhamiria kuendelea kumtumia katika nafasi ya kiungo mshambuliaji nyuma ya Muargentina huyo.

Higuain ni mchezaji ambaye Arsenal sasa wana uhakika wa kumnasa, huku Carlo Ancelotti kocha mpya wa vigogo hao wa Hispania, akitarajiwa kutua leo kuthibitisha kuondoka kwa mchezaji huyo Bernabeu.

Lakini katika uhamisho huo wa Rooney, Arsenal italazimika kumlipa mshahara wake wa Pauni 220,000 kwa wiki, ambao ni mkubwa mno kulingana na tamaduni za Arsenal, imekuwa klabu 'bakhili'.
Wenger haoni kama Rooney ni mshambuliaji wa kati, lakini kama kiunganishi, baina ya kiungo na Higuain — nafasi ambayo mchezaji mwenyewe amesema inamfaa
Lakini Chelsea pia inamtaka Rooney na kocha mpya wa United, David Moyes anatarajiwa kukutana na Rooney wiki mbili zijazo, hivyo uwezekano wa yeye kujiunga na klabu hiyo ya London bado mdogo.
United haitataka kumuuza Rooney kwa Chelsea, ambao wanatarajiwa kuwa washindani wao wakuu katika mbio za ubingwa na matumaini ya mchezaji huyo yanabakia katika kikao chake na Moyes kwamba anaweza kupata mwanzo mpya mzuri Old Trafford, hususan baada ya klabu kusema hajawahi kuomba kuondoka United.
Hilo ni suala lililotokana na wasiwasi wa Rooney juu ya uhusiano wake na mashabiki wa United. Rooney anatarajia kikao kama alichowahi kufanya na kocha aliyetangulia, Sir Alex Ferguson mwishoni mwa msimu uliopita, cha binafasi kujadili mustakabali wake katika klabu. Arsenal imetenga bajeti ya kutosha kupambana katoka soko la usajili, lakini tatizo ni kwamba wataweza kuwashawishi wachezaji wanaowataka, kwa sababu ni wenye kiu ya mataji, vitu ambavyo kwa sasa klabu hiyo vimekuwa adimu

Brazil yaitwanga 2-1 Italia, zatinga nusu fainali kombe la mabara




Neyman akishangilia bao



Neyman akifunga bao







Javier Hernandez amefunga mawili dhidi ya Japan

MABAO ya Dante dakika ya 45, Neymar 55 na mawili ya Fred dakika za 66 na 88 yameipa Brazil ushindi waliostahili wa 4-2 dhidi a Italia usiku wa kuamkia leo na kufuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mabara ikishinda mechi zote katika Kundi A.

Italia ilipata mabao yake kupitia kwa Giaccherini dakika ya 51 na Chiellini dakika ya 71.

Kikosi cha Brazil kilikuwa; Julio Cesar, Dani Alves, Thiago Silva, Luiz/Dante dk33, Marcelo, Gustavo, Hernanes, Hulk/Fernando dk76, Oscar, Neymar/Bernard dk68 na Fred.

Italia: Buffon, Abate/Maggio dk30, Bonucci, De Sciglio, Chiellini, Candreva, Aquilani, Marchisio, Montolivo/Giaccherini dk26, Diamanti/El Shaarawy dk71 na Balotelli.

Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Javier Hernandez alifunga mabao mawli na kukosa penalti Mexico ikiifunga Japan 2-1 na kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye Kundi A. Bao la Japan lilifungwa na Shinji Okazaki na sasa Brazil inaungana na Italia kusonga Nusu Fainali.

Saturday 22 June 2013

IMEVUJA, MIMBA YA PENNY YACHOROPOKA





TAARIFA ya ndani zinazodai kwamba, mimba ya mchumba wa Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nassibu Abdul ‘Diamond’, Peniel Mgilwa ‘Penny’ imechoropoka zimevuja na Risasi Jumamosi imezinasa.

Kwa mujibu wa chanzo makini kilichojitambulisha kwa jina la wifi (jina kapuni) kwa Penny, ni kwamba mtangazaji huyo wa Runinga ya Channel 10 cha jijini Dar hivi sasa hana ujauzito tena kama wengi wanavyodhani.
“Penny hana mimba jamani, yupo fiti kabisa na sidhani hata kama anatarajia kushika ujauzito leo wala kesho,” kilisema chanzo hicho.Hata hivyo, wifi huyo alisema kwamba awali kulikuwa na dalili zilizoonesha kwamba Penny alikuwa ni mjamzito kutokana na mtangazaji huyo kutumia vitu vichachu kama vile maembe na mara kwa mara alikuwa akiumwa hadi kufikia kulazwa hospitali.
Inadaiwa kwamba Penny alipotoka hospitali alionekana kuwa fiti zaidi na hakuwa na dalili zozote za kuwa na ujauzito kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Baada ya gazeti hili kupata habari hizo lililimpigia simu Penny ili kuthibitisha madai hayo:
Risasi Jumamosi: Mambo vipi, Penny pole sana.
Penny: Pole ya nini sasa?
Risasi Jumamosi: Si nimesikia kwamba unaumwa jamani na ukakumbwa na mkasa mwingine?
Penny: Mkasa gani huo unaousema maana mimi niko fiti tu.
Risasi Jumamosi: Nilisikia kwamba baada ya kuumwa na kulazwa hopsitali mimba yako ikatoka?
Penny: (Kimya kwa dakika 3) Asante ni mipango ya Mungu.
Risasi Jumamosi: Sasa unatarajia lini utapata tena mimba nyingine?
Penny :(Kwachuuuuuu). Simu ilikatwa na hata ilipokuwa ikipigwa tena haikuwa ikipokelewa

HIVI NDIVYO ILIVYO KUWA KATIKA SHOW YA MIAKA 13 YA KIKOSI CHA MIZINGA(NEW MSASANI DSM)



Chid Benz akikonga nyoyo za mashabiki wake wakati wa shoo ya Kikosi cha Mizinga kutimiza miaka 13 iliyofanyika katika ukumbi wa New Msasani jijini Dar es salaam.

Chid Benz
Fukuda akichana mistari

Katibu wa CUF, Julius Mtatiro ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza wakati wa shoo maalumkundi la muziki wa Hip Hop la Kikosi cha Mizinga kutimiza miaka 13.


Baadhi ya watu waliotoa mchango mkuwa kwa wasanii wa Kikosi cha Mizinga walipewa vyeti, hapa mwandishi Joseph Zablon akionesha cheti chake baada ya kukabidhiwa ba mgeni rasmi.
Mwakilishi wa Clouds Radio akipokea cheti.


Kala Pina 'Nabii Koko' akitumbuiza





Afande Sele akipagawisha mashabiki.