Sunday 23 June 2013

Brazil yaitwanga 2-1 Italia, zatinga nusu fainali kombe la mabara




Neyman akishangilia bao



Neyman akifunga bao







Javier Hernandez amefunga mawili dhidi ya Japan

MABAO ya Dante dakika ya 45, Neymar 55 na mawili ya Fred dakika za 66 na 88 yameipa Brazil ushindi waliostahili wa 4-2 dhidi a Italia usiku wa kuamkia leo na kufuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mabara ikishinda mechi zote katika Kundi A.

Italia ilipata mabao yake kupitia kwa Giaccherini dakika ya 51 na Chiellini dakika ya 71.

Kikosi cha Brazil kilikuwa; Julio Cesar, Dani Alves, Thiago Silva, Luiz/Dante dk33, Marcelo, Gustavo, Hernanes, Hulk/Fernando dk76, Oscar, Neymar/Bernard dk68 na Fred.

Italia: Buffon, Abate/Maggio dk30, Bonucci, De Sciglio, Chiellini, Candreva, Aquilani, Marchisio, Montolivo/Giaccherini dk26, Diamanti/El Shaarawy dk71 na Balotelli.

Katika mchezo mwingine wa kundi hilo, Javier Hernandez alifunga mabao mawli na kukosa penalti Mexico ikiifunga Japan 2-1 na kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye Kundi A. Bao la Japan lilifungwa na Shinji Okazaki na sasa Brazil inaungana na Italia kusonga Nusu Fainali.

No comments:

Post a Comment