Friday 14 June 2013

MPANGO WA CRISTIANO RONALDO KUREJEA ENLAND WA ONEKANA


cristiano ronaldo



MPANGO wa Cristiano Ronaldo kurejea Ligi Kuu ya England sasa uhai tena baada ya mchezaji huyo mwenye thamani ya Pauni Milioni 80 kukanuisha taarifa za kusaini Mkataba mpya Real Madrid.
Rais wa Real Madrid, Florentino Perez alisema mapema wiki hii kwamba alikuwa anajiamini mchezaji huyo atasaini Mkataba wa kuendelea kuichezea Real, akisema: "Lengo langu, lengo la Cristiano, na lengo la mashabiki wote wa Real Madrid ni kwamba anaendelea kucheza hapa kwa miaka mingi ijayo.’
Pamoja na hayo, akitumia ukurasa wake wa Facebook na akaunti yake ya Twitter, Ronaldo, ambaye amebakiza miaka miwili katika Mkataba wake wa sasa, alisema: "Habari zote kuhusu kusaini kwangu Mkataba mpya Real Madrid ni uzushi,".
Dhahiri klabu yoyote duniani ingetaka kunufaika na uwezo wa Ronaldo baada ya kuzitumikia United na Madrid.
Mkataba wa sasa wa mshambuliaji huyo unamalizika mwaka 2015, lakini amegoma kusaini mpya, Madrid haitakuwa na chaguo lingine zaidi ya kumuuza, ingawa ameunfga mabao mengi kupita kiasi,146 katika mechi 135.
Monaco ilikuwa inaaminika kujiandaa kutoa Pauni Milioni 85 na kumshawishi kwa mshahara babu kubwa ajiunge nao, lakini Ronaldo anaweza kuchagua kurejea Manchester, ambako ameacha kumbukumbu.

Alex Ferguson alikuwa anafikiriwa kuchangia kwa kiasi kikubwa Ronaldo kutorejea katika klabu hiyo, lakini anaweza kuwa na nia ya kwenda katika klabu hiyo ambayo ilimjenga na kuwa mmoja wa wachezaji wakubwa dunian Chanzo na mjengwa.

No comments:

Post a Comment